
MAADHIMISHO ya Siku ya Sheria yamefanyika huku suala la kuchelewa kwa upelelezi wa kesi likitawala ambapo Rais Dk. John Magufuli, Jaji Mkuu na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) wamelizungumzia kwa namna yao.
Suala hilo limetajwa kuchangia watu wengi kukaa mahabusu muda mrefu na kusababisha kupokwa haki zao kinyume na ibara ya 14, 15 (i) na 15 (ii) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais Magufuli ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo jana, aliwanyoshea kidole wapelelezi na kuwataka wabadilike.
“Kila siku wakienda wanasema upelelezi unaendelea, ameshapeleleza, ameshamshika na meno ya tembo huku anazungumza upelelezi unaendelea.
“Ninaomba wapelelezi na wasimamizi wa sheria hili mlifanyie kazi, watu wanateseka, ukienda kwenye magereza watu wanalia na wengine ni kesi za kusingiziwa.
“Wako watu wamewekwa kwa sababu ya matajiri kwamba nakukomesha utakwenda kwanza mahabusu,” alisema Rais Magufuli.
No comments:
Post a Comment