Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Sarakwa wakimsikiliza Naibu Waziri waMaliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu wakati wa mkutanao wa hadhara uliofanyika katika eneo la Shule ya ,msingi ya Sarakwa mara baada ya kusikiliza malalamiko yao kuhusu malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akisalimiana na baadhi ya watumishi wa wilaya ya Bunda mkoani Mara mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mkuu wa wilaya kwa ajili ya kikazi ya siku moja
Mbunge wa jimbo la Bunda vijijini, Boniface Getere akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sarakwa kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu kuzungumzia kuhusu umuhimu wa kutoa taarifa mapema kwenye ofisi za kijiji wakati wanyamapori wakali na waharibifu wanapoharibu mazao yao
Mwenyekiti wa kijiji cha Sarakwa, Samson Kapeta akizungumza na wananchi wake kabla ya kumkaribisha na Mbunge wa jimbo la Bunda vijijini, Boniface Getere kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Sarakwa wakiwa katika mkutano wa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu wilayani Bunda mkoani Mara
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) iunde timu ya kuchunguza uhalali wa malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi kilichotolewa kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori wakali na waharibifu wa mazao katika maeneo mbalimbali nchini.
Mhe. Kanyasu ametoa agizo hilo mara baada ya kupokea malalamiko na madai
kutoka kwa baadhi ya wananchi wa vijiji 4 vinavyopakana na Hifadhi ya
Taifa ya Serengeti, wilayani Bunda mkoani Mara ambao mazao yao yaliliwa
na kuharibiwa na wanyamapori wakali wamekuwa hawalipwi huku
wasiostahili ndo wamekuwa wanalipwa .
Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Sarakwa,
Mariwanda ,Unyali na Kihomboi vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya
Serengeti, Bunda mkoani Mara, Mhe. Kanyasu amesema kuwa mara baada ya
uchunguzi kukamilika wale watakaobainika kupokea fidia hiyo wale
wasiostahili watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kuzirudisha
fedha hizo.
‘’Nataka niwambie, wale waliopokea kifuta jasho na kifuta machozi kutoka serikalini wakati hawastahili lazima hizo fedha wazitapike” Amesisitiza Mhe. Kanyasu
‘’Nataka niwambie, wale waliopokea kifuta jasho na kifuta machozi kutoka serikalini wakati hawastahili lazima hizo fedha wazitapike” Amesisitiza Mhe. Kanyasu
Aidha, Mhe. Kanyasu amesema licha ya fidia hiyo kuendelea kulalamikiwa
kuwa kidogo ikilinganishwa na hali halisi ya maisha ya sasa, wananchi
ambao mazao yao yameharibiwa wanatakiwa kulipwa fidia kwa mujibu wa
sheria iliyopo na sio vinginevyo.
Katika hatua nyingine Mhe. Kanyasu amewataka wananchi wanaoharibiwa
mazao yao na wanyamapori wakali na waharibifu wakiwemo tembo watoe
taarifa ndani ya muda wa siku tatu katika ofisi za vijiji katika maeneo
yao ili hatua za malipo ziweze kufanyika kwa muda.
Pia, Kanyasu amewaeleza wananchi hao kuwa Serikali imeanza kupitia upya
utaratibu wa kifuta jasho na kifuta machozi ili kiweze kuendana na
gharama za maisha ya sasa.
Kwa upande wake Bw. Abel Hadawi, mmoja wa wananchi ambaye mazao yake
zaidi ya ekari 20 yaliharibiwa mwaka jana, amemweleza Naibu Waziri huyo
kuwa amaekuwa akijaza fomu kwa ajili ya kulipwa fidia lakini kila
malipo yanapokuja jina lake limekuwa halimo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) kanda ya Ziwa,
Emmanuel Nkya amewaeleza wananchi hao kuwa wanachotakiwa kufanya ni
kujaza fomu nne ili kuwe na nakala kuanzia ofisi ya kijiji hadi makao
makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii.
Naye Mbunge wa Bunda vijijini, Boniface Getere amemwomba Naibu Waziri
Kanyasu kuyashughulikia malalamiko ya wananchi wote wanaostahili kulipwa
kifuta jasho na kifuta machozi kwa kuwa wengi wao wameathiriwa na
kubaki omba omba kufuatia mazao yao kuharibiwa.
No comments:
Post a Comment