Saturday, 1 December 2018

Afrika Mashariki kutumia sarafu moja



Rais Magufuli na Uhuru Kenyatta

Hilo limewekwa wazi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga jijini Arusha leo Disemba 1, 2018 ambapo amesema mchakato wa kukamilisha sarafu hiyo unaendelea vizuri.
'Sisi wana Afrika Mashariki tunaelekea kuinua uchumi wetu kwa ushirikiano ambapo hatua ya awali tunaanza na kutumia sarafu ya pamoja ambayo itasaidia kwenye hili soko la pamoja tunalolianzisha hivyo ifikapo mwaka 2020 tutakuwa na Umoja wa sarafu kwa kutumia sarafu yetu'', amesema.
Aidha Balozi Mahiga ameweka wazi mipango mbalimbali ya nchi hizo katika kukuza uchumi kwa kutaja maeneo ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi ili kufikia lengo hilo la pamoja.
''Ili kupata maendeleo hapa duniani ni lazima utashi wa kisiasa uwepo, kuondoa vikwazo vya biashara, vikwazo vya mitaji baina ya nchi moja na nyingine pamoja na kupunguza vikwazo vya watu wanaoshirikiana au kutembeleana kwa kuvuka mpaka wa nchi moja kwenda nyingine'', ameongeza.
Mahiga na baadhi ya viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wapo jijini Arusha ambako ulikuwa ufanyike mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya hiyo (EAC), lakini ukaahirishwa baada ya nchi ya Burundi kukosa mwakilishi.

No comments:

Post a Comment