Friday, 7 February 2020

Trump asheherekea ushindi,awaponda wapinzani wake


Trump akiwa ameshika gazeti lililoandika habari ya kusafishwa kwake

Rais wa Marekani Donald Trump amefurahia ushindi baada ya kuondolewa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili, ndani ya Ikulu ya Marekani amewaponda wapinzani wake wa kisiasa.
''Nimefanya makosa kwenye maisha yangu, nitakiri......lakini haya ndio matokeo, '' alisema huku akinyanyua gazeti lililokuwa na kichwa cha habari ''Trump hana hatia''.
''Tumepita kubaya, hatukutendewa haki.Hatukufanya kosa lolote,'' alisema Ikulu. ''Ulikuwa uovu, ilikuwa rushwa.''
'' Sasa tuna neno zuri. Sikufikiria kama litakuwa zuri namna hii, ''Linaitwa kusafishwa kabisa.''

No comments:

Post a Comment