Mfanyibiashara Mohammed Dewji kutoka Tanzania ametajwa kuwa miongoni mwa mabilioni 20 wa Afrika katika ripoti ya jarida la Forbes la mwaka 2020.

Katika ripoti hiyo mfanyabiashara tajiri nchini Nigeria Aliko Dangote ameorodheshwa kwa mara ya tisa mfululizo, kuwa mtu tajiri barani Afrika .
Dangote mwenye umri wa miaka 62 ambaye anafanya biashara ya Simiti, Sukari na unga wa ngano ana utajiri wa dola Bilioni 10.1.
Pia unaweza kusoma:
Dangote anafuatiwa na mfanyabiashara wa Misri Nassef Sawaris ambaye aliongeza utajiri wake kutoka dola bilioni 6.3 hadi dola bilioni nane.
Mfanyabiashara huyo anamiliki asilimia 5.7 katika kmapuni ya viatu ya Adidas . Ongezeko la hisa za Adidas liliomuongezea dola bilioni moja nukta tano katika akaunti yake.
Orodha ya mbilionea 20 na utajiri wao barani Afrika:
- Aliko Dangote $10.1 B
- Nassef Sawiris $8 B
- Mike Adenuga $7.7 B
- Nicky Oppenheimer $7.7 B
- Johann Rupert $6.5 B
- Issad Rebrab $4.4 B
- Mohamed Mansour $3.3 B
- Abdulsamad Rabiu $3.1 B
- Naguib Sawiris $3 B
- Patrice Motsepe $2.6 B
- Koos Bekker $2.5 B
- Yasseen Mansour $2.3 B
- Isabel dos Santos $2.2 B
- Youssef Mansour $1.9 B
- Aziz Akhannouch $1.7 B
- Mohammed Dewji $1.6 B
- Othman Benjelloun $1.4 B
- Michiel Le Roux $1.3 B
- Strive Masiyiwa $1.1 B
- Folorunsho Alakija $1 B
No comments:
Post a Comment