Sunday, 28 April 2024

Barabara yamogoka kimazichana safari Lindi, Mtwara na Kwingineko hatarini

Wakazi wa Kimazichana Mkoani Pwani wamefikwaa na hadha ya kumogoka kwa sehemu ya barabara kuu inayounganisha maeneo mbalimbali ikiwemo mikoa ya kusini mapema hii leo.

Akizungumza na mtanzania digital shuhuda wa tukio hilo aliyejitambulisha kuwa Mudhihiri Muhsin kutoka eneo hilo amesema kuathirika kwa barabara hiyo ni kutokana na mvua zinazoendelea Kunyesha Huku akisema kiasi kingi cha mvua iliyonyesha alfajiri ya kuamkia leo ndiyo imepelekea madhara hayo.

PICHA MBALIMBALI ZIKIONESHA HALI HALISI YA ATHARI ZILIYOJITOKEZA


Kamati ya uongozi yaridhishwa usimamizi wa mradi JNHPP

Kamati ya Uongozi wa Mradi wa Julius Nyerere ulio chini ya Mwenyekiti Mhandisi Cyprian Luhemeja ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu Rais Muungano na Mazingira wametembelea Bwawa la kufua umeme wa Maji wa Julius Nyerere (JNHPP) katika mto Rufiji kwa lengo la kujionea maendeleo ya Mradi huo unaotarajia kuzalisha Megawati 2115 za umeme

Viongozi hao wakiongozwa na Mwenyekiti Mhandisi Luhemeja, walitembelea mradi huo Aprili 27,2024 ambapo katika ziara hiyo waliambatana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio.

Baada ya Kutembelea Bwawa la Julius Nyerere Mhandisi Cyprian alisema wamefurahishwa na namna wataalamu wa Kitaanzania walivyoweza kusimamia mradi huo kwa ustadi mkubwa.

Amewasisitiza wataalamu wanaotekeleza mradi huo kuwa watanzania wanahitaji kupata huduma ya umeme wa uhakika.

“Najuwa kazi kubwa imefanyika na serikali imewekeza fedha nyingi hivyo watanzania wanatarajia kupata umeme wa uhakika muda si mrefu,” alisema.

Aidha, aliwapongeza Wizara ya Nishati, Shirika la Umeme ( TANESCO) na wadau wengine kwa kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa ufasaha.

Dkt. Biteko: Shule Binafsi zizingatie maadili ya Mtanzania

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi hususan shule binafsi ili kuboresha sekta ya elimu nchini.

Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Shule Binafsi Nchini (TAPIE), leo Aprili 27, 2024 jijini Dar es salaam Dkt. Biteko amesema kuwa Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan haiwezi kuacha Wadau wa Elimu wakilalamika, kwa kuwa uwepo wao unaisaidia Serikali.

“Nataka niwahakikishie kuwa Serikali imeendelea kukutana na TAPIE mara kwa mara, na hapa namuelekeza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Jenista Mhagama kuratibu mkutano wa pamoja kati ya TAPIE na Wizara za Ardhi, Fedha, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili kujadiliana kwa pamoja na kupata suhulu ya changamoto zinazowakabili,” amesema Dkt. Biteko.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amewaasa TAPIE kuzingatia masharti yaliyoainishwa katika barua na vyeti vya usajili wa asasi zao, kwa kuwa kuna baadhi hukiuka masharti hivyo kusababisha migongano isiyo ya lazima na mamlaka zilizokasimiwa kusimamia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya uendeshaji wa asasi za elimu nchini.

Vilevile, amewataka kufuata sheria na kanuni za utoaji elimu, kuhimiza na kuimarisha maadili, nidhamu na malezi bora kwa watumishi na wanafunzi walio chini ya asasi zao. Pia, amesema kuwa suala la uadilifu katika shughuli za uendeshaji na usimamizi wa mitihani ya Kitaifa lisisitizwe na kutiliwa mkazo ili kupata wataalam wenye sifa stahiki.

Naye, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amezipongeza shule binafsi kwa kufanya uwekezaji mkubwa ambao sasa unavutia baadhi wanafunzi kutoka nchi zingine kuja kusoma hapa nchini

“Tunapozungumza kuwa tunaenda na elimu ya miaka 10 tunaamini sekta binafsi ina msaada mkubwa katika hili kwa sasa tutanza na ujenzi wa shule 100 za sekondari za ufundi na ni imani yangu kuwa tutashirikiana vizuri na sekta binafsi,” amesisitiza Prof. Mkenda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Husna Sekiboko amesema kuwa Serikali imeweka mazingira wezeshi katika sekta binafsi na sasa kuna zaidi ya shule 500. Pia, amempongeza Rais Mhe. Dkt. Samia kwa kutoa maelekezo ya kuboresha sekta ya elimu nchini.

“Tunaipongeza sekta binafsi kwa kutoa ajira na Bunge tunatambua mchango wa TAPIE, tutawaunga mkono katika kuboresha sekta hii ya elimu. Kuhusu leseni ya kuanzisha shule, Kamati yangu inaungana na TAPIE tunaoomba Serikali izungumze na wadau ili kusaidia kupiga hatua ya utekelezaji wa mitaala iliyowekwa,” ameeleza Sekiboko.

Aidhs, meitaka TAPIE kulinda mikataba ya watumishi walio chini ya Taasisi zao ikiwa ni pamoja na kuwasilisha michango yao katika Mifuko ya Hifadhi za Jamii.

Wizi Rufiji: 11 washikiliwa kwa mahojiano, wamo watendaji wa Serikali


Watendaji wa Kata, Kijiji pamoja na vibarua tisa waliokua wakifanya shughuli ya kupokea misaada ya waliokumbwa na mafuriko wilayani Rufiji wanashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa – TAKUKURU, kwa tuhuma za wizi wa vyakula vya misaada inayotolewa na serikali na Wahisani mbalimbali kwa watu waliokumbwa na mafuriko Wilayani humo.

Akielezea tukio hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya maafa ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Eward Gowele amesema watuhumiwa hao wanashikiliwa TAKUKURU kwa mahojiano huku akiwaonya wanaopewa dhamana ya kusimamia misaada hiyo kutojihusisha na wizi wa misaada hiyo.

Alisema, wapo Mtendaji wa Kata na Kijiji ambao walikiuka miongozo kwa kutoa chakula au kwa kujigawia chakula nje ya utaratibu huku wakijua wazi wao sio waathirika wa mafuriko na tayari wamechukuliwa hatua ambapo TAKUKURU wanaendelea na uchunguzi dhidi yao.

“Pia wapo vijana ambao tunawatumia kwa kazi za vibarua wa kushusha mizigo nao walifanya hivyo TAKUKURU waliwakamata vijana hao tisa ambapo wanaendelea kushughulika nao kwa mujibu wa sheria,” alisema Meja Gowele.

Saturday, 27 April 2024

BAKWATA Katavi wazindua mfumo matumizi ya Tehama.

 Baraza Kuu la Waislam Tanzania – BAKWATA, Mkoa wa Katavi limezindua mfumo wa matumizi ya TEHAMA katika shughuli mbalimbali za kiofisi, uliogharimu zaidi ya shillingi milioni 2.5

Katavi, unakuwa mkoa wa kwanza nchini kuanza kuutumia mfumo huo tangu kuzinduliwa na mufti mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeir.

Akizindua mfumo hu, Meneja wa Benki ya TCB, Chacha Petri amepongeza hatua hiyo ya BAKWATA kuingia kwenye matumizi ya TEHEMA na kueleza kuwa huo ndio mfumo wa kisasa ambao taasisi makini inapaswa kuutumia.

Katika hatua nyingine Chacha ameahidi kutoa vifaa ikiwemo kamera na kompyuta mpakato (laptop) kwa BAKWATA Mkoa wa Katavi kama moja ya njia ya kuendalea kuimarisha matumizi ya TEHAMA kwa taasisi hiyo.

Sheikh wa Mkoa wa Katavi, Mashaka Kakulukulu amesema mfumo wa TEHAMA ni moja kati ya hatua za mabadiliko ndani ya BAKWATA chini ya mufti mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir wa kutaka wailam kutoachwa nyuma na Teknolojia.

Uzinduzi wa mfumo huo umejumuisha ugawaji wa vishikwambi vinne (4) ambavyo vitasaidia kuendesha mfumo wa TEHAMA katika ofisi ya BAKWATA mkoa wa Katavi, Ofisi 3 za BAKWATA Wilaya za Mpanda, Tanganyika na Mlele na Printa moja kwa ajili ya ofisi ya Mkoa.

Mwenge wabaini madudu mradi wa Maji Malinyi


Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2024 Godfrey Mzava ameeleza kutoridhishwa na utaratibu uliotumika kukamilisha uboreshaji wa mradi mkubwa wa Maji wa Sofi Mission, uliopo Wilayani Malinyi baada ya kubaini kuwepo kwa uzembe wa ufatiliaji na mapungufu katika ulipaji wa kodi na matumizi ya mfumo wa manunuzi kwa njia ya kidigitali NeST.

Uboreshaji wa Mradi huo ni pamoja na ujenzi wa tenki la maji lenye ujazo wa lita 150,000 kwenye mnara wenye kimo cha mita sita, ufungaji wa mfumo rahisi wa kutibu maji, uboreshaji wa vituo 11 vya kuchotea majina ujenzi wa uzio kwa gharama ya shillingi 156,955,962 chini ya Mkandarasi wa Dar es Salaam.

Awali, akisoma taarifa Kwa kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa ,Meneja wa RUWASA wilaya ya Malinyi Mhandisi Marco Chongero amesema Mradi huo tayari umeanza kutoa huduma kwa wananchi.

Kagera: Wanawake zaidi ya 400 wakutwa na maambukizi ya Saratani


Takribani Wanawake 347 wamebainika kuwa na maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi, kati ya wanawake 4689 waliyofanyiwa uchunguzi wa maradhi hayo Mkoani Kagera.

Mganga Mkuu wa Mkoa Kagera, Dkt. Samwel Laizer ameeleza hayo katika kilele cha chanjo Afrika kimkoa, kilichofanyika Manispaa ya Bukoba kwa kuambatana na uzinduzi wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi (HPV).

Dkt. Laizer amesema Mkoa Kagera ni miongoni mwa mikoa inayoathiriwa na magonjwa yanayodhibitiwa kwa chanjo ikiwemo saratani ya mlango wa kizazi kwasababu takwimu za mwaka 2023/2024 zinaonesha kiwango kikubwa cha ongezeko la wagonjwa wa saratani ya HPV.

“Kwa mwaka 2023 zinaonyesha wanawake waliyofanyiwa uchunguzi wa saratani ya mlango wa 17668 na kubaini kuwa wanawake 469 wana mambukizi ya ugonjwa huo na mwaka huu kwa kipindi cha January 2024 wanawake 4689 wamefanyiwa uchunguzi na kubaini 347 kuwa na maambukizi ya HPV,” alisema.

Naye Abdoni Kawha ambaye  alimwakilishi Afisa Elimu Mkoa Kagera kwenye uzinduzi wa wa chanjo ya HPV, amesema jumla ya Wanafunzi 17600 kutoka shule 362 watashiriki chanjo hiyo na wamejipanga vizuri kuhakikisha walengwa wote kutoka shule hizo wanafikiwa kama ilivyo mpango wa Serikali.

Hata hivyo, Mratibu wa chanjo Mkoa Kagera, Salimu Rajab Kimbao amesema wamepokea dozi 299,040 ambazo tayari wamezifikisha katika vituo vyote vya afya Mkoani humo kwa ajili ya kuwakinga walengwa wote na kwa kila Halmashauri uzinduzi unaendelea na huduma ya kutoa chanjo ukiwa unanalenga kufikia asilimia 90.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Bukoba Erasto Sima, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa Kagera Hajath Fatma Mwasa amewataka wataalamu wote watakaohusika kwenye zoezi hilo kuhakikisha wanafika kwenye vituo na maeneo waliyopangiwa kufanya kazi pamoja na kusimamia na kutumika vifaa ipasavyo.

Wednesday, 12 May 2021

WAFANYAKAZI WA BENKI YA I&M WAMETOA MSAADA WA VITU MBALIMBALI KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA – KIGAMBONI, DAR ES SALAAM.

 

Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiwa na baadhi ya watoto wa kituo hicho
Bi.Anitha Pallangyo, meneja masoko Benki ya I&M wapili kushoto akikabidhi baadhi ya zawadi walizopeleka kwenye kituo hicho cha watoto yatima
Timu ya Benki ya I&M leo walipotembelea kituo cha yatima chini ya mpango wao wa kujitolea wa 'IM for You' kushoto ni Bi. Hellen Mbwana, afisa wa benki kitengo cha ukaguzi, Anitha Pallangyo, meneja masoko, Mlekwa Augustine, huduma kwa wateja, Theresia Nguma kitengo cha malipo, fedha na biashara, na Debora mwakyoma afisa masoko na mawasiliano ya benki.

 Timu ya wafanyakazi wa I&M walipotembelea kituo cha watoto yatima cha Lady Fatema kilichopo Mjimwema mageti saba, kigamboni Jijini Dar es salaam.

DAR ES SALAAM. Wafanyakazi wa Benki ya I&M Tanzania siku ya Jumanne tarehe 11, Mei, 2021, wamejitolea msaada wa vitu mbalimbali kama vile vyakula, nguo, sabuni pamoja na vifaa vya shule katika moja ya kituo cha kulea watoto yatimakiitwacho ‘Lady Fatema’  kilichopo Mjimwema mageti saba, Kigamboni Jijini Dar es salaam chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii kupitia mpango huo ambapo wafanyakazi hujitolea kwa jamii kwa njia mbalimbali kama vile kutoa elimu ya fedha na ujasiriamali kwa wanawake na vijana ili waweze kujiajiri pamoja na kusaidia vitu mbalimbali kwa wahitaji.

Wasimaizi wa kituo hicho Bi. Mariam Ramadhan na mmewe Bw. Kalekela Omari Mahmood walianzisha kituo hicho mnamo mwaka 2011 wakiwa na lengo la kusaidia watoto yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi wakiwapatia elimu, chakula na hifadhi ya kulala. Mbali na misaada mbalimbali inayopelekwa na wafadhili, kituo hicho kina changamoto ya eneo la kutosha la kuweza kuhifadhi watoto wengi na wa jinsia tofauti kwani kwa sasa imewalazimu kubaki na jinsia ya kiume tu kutokana na ukosefu wa vyumba vya kutosha kwaajili ya watoto hao.

Katika kuadhimisha mwezi mtukufu wa Ramadhani na ikiwa ni wiki ya kuelekea sikukuu ya Eid Al-Fitr, wafanyakazi wa benki ya I&M waliamua kujitolea vitu hivyo katika kituo cha kulea watoto yatima Mjimwema Kigamboni ili na wao waweze kusheherekea na kufurahia sikukuu ya EID inayotarajiwa kuwa mwishoni mwa wiki hii kutegemeana na kuandama kwa mwezi. Vilevile wafanyakazi wa benki ya I&M waliweza kuwapa elimu ya usimamizi wa fedha na ujasiriamali kwa vijana na wanawake waliokuwa katika kituo hicho ili iweze kuwasaidia katika usimamizi wa fedha za kituo hicho pamoja na kijiajiri wao wenyewe pindi watakapoanza kujitegemea.

Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kwa kufundisha wanawake, vijana na wajasiriamali katika kikundi cha Wanawake wajasiriami kilichopo Yombo vituka, Temeke jijini Dar es salaam, vilevile wiki iliyopita wafanyakazi wa benki hiyo walijitolea damu  ili kusaidia wagonjwa wenye uhitaji wa damu katika hospitali ya Taifa ya Muimbili.

Monday, 3 May 2021

I&M Holdings PLC Completes Acquisition of Orient Bank Limited in Uganda

 


 Nairobi/Kampala, 3rd May, 2021: I&M Holdings PLC has announced the majority acquisition of Orient Bank Limited (OBL) from 8 miles LLP and Morka Holdings Limited. OBL is the 12th largest bank and a licensed and established commercial bank in Uganda.
I&M Holdings PLC and Orient Bank Limited signed an agreement in July 2020 for I&M Holdings PLC to acquire 90 percent shareholding of the Ugandan entity. The acquisition was completed on 30th April 2021 after receiving the necessary approvals from the Central Bank of Kenya, Bank of Uganda, Capital Markets Authority of Kenya and the COMESA Competition Authority.
The move underscores I&M Group’s commitment to its growth and expansion strategy in Eastern Africa, where Uganda was the missing link in the Group’s strategic effort to set up its presence in all East African countries.  A key focus of this strategy is to seek opportunities to invest at a local and regional level enabling the Bank to serve the needs of all customers, while promoting trade flows within the region.
This development supports the Group’s Business Growth initiatives through diversification of revenue streams by entry into new markets and extension of its Corporate, Business, Personal Banking, as well as Treasury and Trade Finance solutions, to all its customers operating in Uganda.
Commenting on the acquisition, I&M’s Group Executive Director, Sarit Raja Shah noted, “I&M Group aspires to be Eastern Africa’s leading financial partner for growth.  The acquisition of OBL will place I&M Bank in an advantageous position to capitalise on the growth in the Eastern African economies and thereby ultimately increasing shareholder value.”
“This acquisition is expected to give the Group greater capacity to grow profitably, through extending our network to our Regional customers. Further it demonstrates our continued leadership role in the industry across East Africa”, Sarit Raja Shah added.
Dr. Ketan Morjaria, a founding member of OBL and continuing shareholder and Director said “This acquisition marks a great milestone in the history of Orient Bank. We are proud to be integrating into a regional group like I&M Holdings PLC and this synergy will allow our customers to benefit from more seamless and superior banking products whilst continuing our tradition of trust.”
Kumaran Pather, CEO of OBL said “The acquisition of OBL into I&M Holdings PLC will see the new entity rise to greater heights and allow us to broaden our market reach and penetration. The management of OBL are excited to be part of a large and
fast growing Group and look forward to serving new and existing customers alike with better products, digital platforms and regional services.”    
Through the acquisition, I&M Group has acquired additional net loan assets of approximately KES 7.7 Billion, deposits of KES 18.2 Billion, a customer base of close to 70,000, a staff component of 340 employees and a network of 14 branches and 22 ATMs across the country.
A clear plan for the integration of OBL has been developed and through its execution the Group expects to gain considerable business and operational synergies.
I&M Group has made significant investments in its robust infrastructure as part of its digital transformation journey. Through this acquisition, OBL customers will now benefit from this technologically driven infrastructure, which will give them a wide suite of market driven financial solutions aimed at meeting their financial and lifestyle requirements.  
The I&M Group will continue to focus on mergers and acquisitions as part of its growth strategy, as we continue to enhance our shareholders’ value and to provide our customers with a wide network of banking solutions across the region.
The transaction with OBL adds to a list of previous strategic alliances that the Group has effectively completed such as the acquisition of Giro Commercial Bank Limited in Kenya, I&M Burbidge Capital Limited in Kenya and Uganda, CF Union Bank in Tanzania, BCR Bank in Rwanda and First City Bank in Mauritius. We believe that our aspiration in becoming Eastern Africa’s leading financial growth partner is well on course.
In his concluding remarks, Mr. Sarit Raja Shah, noted, “Uganda has made great strides in improving access to financial services across the country. The partnership with Orient Bank Limited is very timely since the Group plans to play a significant role in the growth of the banking sector in Uganda, as it has done in other East African markets.”

Saturday, 1 May 2021

WAFANYAKAZI WA I&M BANK WAJITOLEA DAMU KUOKOA MAISHA YA WATANZANIA WAKISHIRIKIANA NA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

 

Meneja masoko na mawasiliano benki ya I&M Tanzania kushoto Bi.Anitha Pallangyo akiwa na wafanyakazi wenzie katika kampeni ya uchangiaji dau
         Damu ikiendelea kutolewa kutokana na hamasa iliyoletwa na wafanyakazi wa Benki ya I&M
   Mkuu wa kitengo cha mikopo Bw.Clemence Kagoye wa benki ya I&M akiwa anatoa damu katika kampeni ya kuchangia damu ilioandaliwa na benki hiyo
    Bi.Lencer Odhiambo kutoka kitengo cha huduma kwa wateja cha benki ya I&M akiwa anajitolea damu katika kampeni ya kuchangia damu   
 

Mwandishi Wetu

Benki ya I&M Tanzania, Ijumaa tarehe 30 Aprili 2021, walifanya Kampeni ya utoaji Damu ili kuokoa maisha ya watanzania chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii. Kampeni hiyo ilifanyika Makao Makuu ya Benki hiyo yaliopo Maktaba Square jijini Dar es salaam.

Zaidi ya wafanyakazi 30 walishiriki na kujitolea Damu ili kuiwezesha Serikali kukabiliana na upungufu wa Damu kupitia hospitali ya taifa ya Muhimbili ambayo ilishirikiana na Benki hiyo katika zoezi la utoaji damu.

Kwasababu uhitaji wa damu bado upo, Benki ya I&M kupitia mpango wake wa ‘IM FOR YOU’ ambao wafanyakazi wake hujitolea kwa jamii wameamua kufanya kampeni hii ya uchangiaji damu kama njia ya kurudisha kwa jamii.

Akiongea wakati wa zoezi hilo la kujitolea damu, Bi. Anitha Pallangyo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M alisema,”tumefurahishwa sana na muitikio ambao wafanyakazi wenzetu wameonyesha katika zoezi hili la kipekee. Tunawashukuru sana hospitali ya Taifa  Muhimbili kwa muitikio wao walioonyesha kwa kukubali kushirikiana nasi katika zoezi hili la utoaji damu ili kuokoa maisha ya watanzania wengi wenye uhitaji wa damu.”

 Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Kitengo cha Uboreshaji huduma za Benki Bi. Deepali Ramaiya, , Alisema “Hii ni moja ya mipango mikakati ya aina yake ambayo huanzishwa  na wafanyakazi wenyewe wa Benki ya I&M, kwa kujitolea huduma bure kwa jamii kama vile kutoa Elimu ya Ujasiriamali bure kwa wafanyabiashara kupitia Vikundi mbalimbali na sasa wamejitolea damu kupitia Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

 Naye Afisa muhamasishaji damu kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,John Daniel Bigambalaye alisema, “sisi kama wawakilishi wa Muhimbili kitengo cha damu, tumehamasika na kampeni hii iliyoandaliwa na wafanyakazi wa Benki ya I&M kwa jitihada hizi za kusaidia hospitali ya Taifa na watanzania wenye uhitaji wa damu kwa ujumla. Tunashauri na taasisi nyingine ziwe mstari wa mbele katika kuhamasisha wafanyakazi wake kujitolea kwa jamii”

 Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kufundisha Wanawake, Vijana na Wajasiriamali, kujitolea damu  na mengine mengi kwenye sekta ya Afya, Elimu na Mazingira.

 Licha ya wafanyakazi wa Benki ya I&M kujitolea damu pia walialika Taasisi mbalimbali na kampuni zilizo karibu na Makao Makuu ya Benki ili kushiriki.

Tuesday, 27 April 2021

KAMATI YA MAKATIBU WAKUU YAANDAA MKAKATI KABAMBE WA KUBORESHA MICHEZO MASHULENI

 


Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye dhamana yaElimu,Michezo na TAMISEMI  wakiwa kwenye kikao kazi leo Aprili 27,2021 Jijini Dodoma kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa Mkakati wa Utekelezaji wa masuala mbalimbali ya uimarishaji wa somo la Elimu kwa Michezo na Michezo katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini chini ya uenyekiti wa Prof.Riziki Shemdoe ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya  TAMISEMI.


Dkt. Hasssan Abbasi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia eneo la Elimu ndugu  Gerard Mweli (kulia) wakihudhuria kikao cha Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye dhamana ya Elimu, Michezo na TAMISEMI  wamefanya kikao kazi leoAprili 27,2021Jijini Dodoma kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa Mkakati wa Utekelezaji wa masuala mbalimbali  yauimarishaji wa somo la Elimu kwa Michezo na Michezo katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini. Upande wa pili ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Yusufu Omary Singo

 

Na John Mapepele, Dodoma

Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye  dhamana ya Elimu, Michezo na TAMISEMI  wamefanya kikao kazi leo Aprili 27,2021 Jijini Dodoma kujadili  utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri  wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa  Mkakati  wa Utekelezaji wa masuala  mbalimbali  ya uimarishaji wa somo la Elimu kwa Michezo na Michezo katika shule za Msingi na Sekondari  hapa nchini

Mwenyekiti wa Kikao hicho, Prof. Riziki  Shemdoe  ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI amesema  miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa  na kukamilika ni pamoja na   kuandaliwa kwa  mapendekezo ya uimarishaji wa ufundishaji wa somo la michezo shuleni na tahasusi zenye somo hilo kwa kidato cha tano  ambapo ameseme tahasusi hizo zitaanza kufundishwa katika mwaka huu wa masomo.

Pia rasimu ya Mpango Mkakati na Mikakati ya utekelezaji wa masuala mbalimbali ya  somo  la Elimu kwa michezo na michezo katika shule za Msingi na Sekondari  imeandaliwa ili  kuboresha  michezo mashuleni.

Kuhusu kuandaa kiunzi cha uendeshaji wa michezo ya UMITASHUMTA na UMISSETA  Prof. Shemdoe amesema  tayari  Kamati ya Wataalam imeshauri kuwa  kwa sasa  miongozo iliyopo itumike na kiunzi tayari kimeshaandaliwa kwa kuzingatia changamoto  zilizopo ambapo  kitajadiliwa  na wadau wote Juni mwaka huu wakati wa michezo ya UMISHUMTA NA UMISSETA na  kwa sasa tayari miongozo hiyo imeshatumwa kwenye  mikoa yote hapa nchini.

Aidha, suala la uundwaji wa Kamati ya kitaifa ya UMISHUMTA NA UMISSETA tayari imependekezwa na kukubalika kuundwa kwa Kamati ya Usimamizi itakayoundwa na wataalam wawili wawili kutoka kwenye kila Wizara ambapo imekubalika kuwa  pamoja na usimamizi, Kamati itatumia fursa hiyo kujifunza na kuangalia changamoto zilizopo kwenye uendeshaji wa michezo ya UMITASHUMTA  na UMISSETA kuandaa  mapendekezo yatakayojadiliwa  na wadau wote kwa ajili ya  maboresho zaidi.

Prof. Shemdoe amesema kuhusu mchakato wa maandalizi ya UMISHUMTA NA UMISSETA mwaka huu, tayari mikoa yote imeshaandikiwa barua ya taarifa na Mhe. Waziri Ofisi ya Rais –TAMISEMI na kwamba waratibu wa michezo wanakwenda kwenye ukaguzi wa viwanja na maeneo ya malazi na chakula kuanzia Aprili 28-30, mwaka huu. Pia Kamati ya wataalam inaendelea na ufuatiliaji wa Shule teule za michezo ili kuhakikisha kuwa michezo inafanyika kwenye kiwango kinachotakiwa.

Makatibu Wakuu walioshiriki  kwenye  kikao hiki ni pamoja Mwenyekiti wa kikao hicho, Prof. Riziki  Shemdoe  ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI,na Naibu wake  anayeshughulikia eneo la Elimu ndugu  Gerard Mweli, mwingine ni  Dkt. Hasssan Abbasi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Dkt. Leonard Akwilapo  kutoka  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojioa pamoja na Watendaji mbalimbali kutoka  Wizara hizo.

Maelekezo  ya Mawaziri wenye dhamana ya elimu, Michezo na TAMISEMI yalitolewa wakati wa kikao cha pamoja kilichofanyika Februari 8, Mwaka huu.

Tuesday, 20 April 2021

SERIKALI YAANZISHA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KUENDELEZA VIPAJI VYA MICHEZO.

 


 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusuph Singo Omari (kushoto), akiwa naa liyewahi kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF na Kocha wa Timu ya Taifa Stars, Ami Ninje (katikati) na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya Dkt. Richard Masika wakikagua eneo la chuo kwa ajili ya mradi wa upanuzi wa chuo hicho ili kujenga Kituo cha kuendeleza vipaji vya michezo.

Timu ya wataalam mbalimbali wa michezo na ardhi ikipitia ramani ya maeneo ya ujenzi wa madarasa na hosteli.

Timu ya wataalam ikiangalia eneo la ujenzi wa madarasa wa Kituo cha kuendeleza vipaji vya Michezo

 



Na John Mapepele, Dodoma

 

Serikali inatekeleza mradi wa  kupanua eneo la  Chuo cha  Maendeleo ya Michezo Malya ikiwa ni  mkakati  maalum wa kuanzisha Kituo cha Kuendeleza Vipaji vya Michezo  ili kuibua na kuendeleza vipaji vya wanamichezo hapa nchini.

 

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusuph Singo Omary ameyasema haya  wakati alipokuwa na  Timu ya wataalam walipotembelea na kukagua eneo  hilo hivi karibuni ikiwa ni sehemu ya kufanya maandalizi ya ujenzi wa kituo hicho ambacho kitakuwa na hadhi ya kimataifa.

 

“Niseme tu kwamba  kukamilika kwa kituo  hiki kutaifanya  nchi yetu kusonga mbele kwenye  Sekta ya Michezo kwa kuwa  vipaji vya wanamichezo wetu vitaibuliwa na  tutaweza sasa  kushindana  na mataifa mengine duniani sasa” amefafanua Mkurugenzi Omary

 

Amesema Tanzania ina hazina kubwa ya vipaji kilichokuwa kinakosekana ni kituo maalum cha michezo cha kuwanoa wachezaji na kwamba kukamilika kwa kituo hiki ni suluhisho la kudumu la changamoto hiyo.

 

Awali, Katibu Mkuu wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi amesema  Wizara imeendelea  kufanya mageuzi makubwa ili kutimiza ahadi  za Serikali na matarajio ya wananchi kwa ujumla.

 

Amesema Wizara  inatekeleza kwa kwa kasi  masuala yote  yaliyobainishwa kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka  2020-2025 ikiwemo ibara125(a)-(h) kwa Sekta ya Habari, ibara239 (a)-(m) kwa Sekta ya Utamaduni, ibara 249 (a)-(j) Sekta ya Sanaa na ibara 243(a)-(k) kwa Sekta ya Michezo.

 

Akihutubia kwenye kikao cha Wafanyakazi wa wa Wizara hiyo hivi karibuni, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amesema tayari Wizara yake imeshakamilisha agizo la Serikali la kuanzisha Mfuko wa Sanaa na Utamaduni ikiwa pia ni mkakati wa kukuza sekta ya Michezo nchini.

 

“Wizara imekamilisha agizo hili kwa kuhuisha Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa na Utamaduni ambao umetengewa shilingi bilioni 1.5. 

Mfuko  huu kwa  mwaka ujao wa fedha utajikita katika ujenzi wa miuondombinu muhimu ikiwemo jengo la SANAA HOUSE hapa Dodoma, pia utaendelea  kutengewa fedha zaidi kwa lengo la kutekeleza  majukumu mawili adhimu; kuwajengea uwezo wanatasnia hizo za Sanaa na Utamaduni kupitia mafunzo na  kuwawezesha kupata mikopo na ruzuku katika kazi zao” amesisitiza Waziri Bashungwa

Wednesday, 14 April 2021

MAWAZIRI WATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA SULUHU KIKAMILIFU

 


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Pauline Gekul (kushoto) akizungumza leo katika kikao cha Mawaziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na Wizara hiyo cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu ya Sekta hizo ya kisera, kisheria na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchini kilichofanyika jijini Dodoma, anayefuata ni Waziri wake Innocent Bashungwa akifuatiwa na Waziri waMawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Faustine Ndugulile na kuliani Naibu wake Mhandisi Kundo Mathew.

Kikao hicho kimefanyika kufuatia maelekezo yaliyotolewa hivi karibuni na Mheshimiwa  SamiaSuluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  yakutaka kufanyika marekebisho ya Sheria na Kanuni zinazosimamia Vyombovya Habari  hapa nchini hususan Televishen Mtandao (Online TV)

 

Wajumbe wa kikao cha Mawaziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja naWizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas akizungumza katika kikao hicho cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu yaSekta hizo ya kisera, kisheria  na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchini kilichofanyika jijini Dodoma leo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas (kushoto), akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Zainab Chaula akifuatiwa na Naibu wake Dkt. Jim Yonaz katika kikao cha Mawaziri wa Wizara hizo mbili cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu ya Sekta hizo ya kisera, kisheria na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchin ikilichofanyika jijini Dodoma leo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas (kushoto) akizungumza leo katika kikao cha Mawaziri wa Wizara hiyo na Wizara ya Mawasiliano naTeknolojiaya Habari cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu ya Sekta hizo yakisera, kisheria na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchini kilichofanyika jijini Dodoma.Kulia ni Katibu Mkuu waWizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Zainab Chaula. Kikao hicho kimefanyika kufuatia maelekezo yaliyotolewa hivi karibuni na Mheshimiwa SamiaSuluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yakutaka kufanyika marekebisho ya Sheria na Kanuni zinazosimamia Vyombo vya Habari hapa nchini hususani Televishen Mtandao (Online TV)

 

Na John Mapepele, Dodoma

Waziri anayesimamia Sekta ya Habari Mhe. Innocent Bashungwa na Waziri anayesimamia Sekta ya Mawasiliano Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile na timu ya Makatibu  Wakuu na Wataalam  wa Wizara hizo  wamekaa na kujadili  hoja mbalimbali kuhusu  utekelezaji wa Sera, Sheria na Kanuni za kisekta kufuatia  maelekezo  ya hivi karibuni ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Maelekezo hayo aliyatoa   wakati wa  kuwaapisha Makatibu Wakuu, Naibu  Makatibu  Wakuu na  Wakuu wa Taasisi ya kufanya marekebisho ya Sheria na Kanuni  zinazosimamia Vyombo vya Habari hususan Televisheni Mtandao (Online TV).

Majadiliano hayo yamefanyika jijini Dodoma Aprili 14, 2021 na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa kwenye hoja 13 zilizoainishwa na Wizara hizo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa  amesema miongoni mwa  maazimio  yaliyofikiwa ni pamoja na kufanya  mapitio ya Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo katika maeneo yote yenye mapungufu  ili ziendane na  hali halisi ya sasa  na  kuweka  mifumo rafiki ya kushughulikia masuala  yote  yanayohusu sekta ya  Mawasiliano na Utangazaji

“Tumeagiza Wataalam wafanye uchambuzi wa Kanuni za Maudhui Mtandaoni ili kuona kama zinaendana na mazingira ya sasa” amesisitiza Waziri Bashungwa

Ameongeza kuwa Wizara zimeaazimia kuja na mkakati wa kuwaelimisha  wadau wa Sekta hizo ili kudhibiti makosa  ya kimaudhui  yanayofanywa  na Vyombo vya Habari badala ya hali ilivyo sasa inayotoa adhabu kali zinazojikita kwenye utozaji wa faini kubwa pamoja na kufungiwa.

Suala lingine ambalo limeazimiwa kufanyiwa kazi ni chaneli za bure kutoonekana kwenye visimbusi ambavyo kimsingi zinapaswa kuonekana hata pale kifurushi kinapokuwa kimeisha muda wake.

Kwa upande wake Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine  Ndugulile amesema kukua kwa teknolojia kumewezesha kukua kwa matumizi ya huduma za mawasiliano yakiwemo ya utangazaji hivyo katika kipindi kifupi  kijacho Serikali  kupitia  Wizara hizo mbili  itafanya  maboresho  makubwa  kwenye kanuni husika ili kuendana na  hali halisi ya sasa.

 

Ameongeza kuwa Serikali ilitunga Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali zikiwemo Sheria ya huduma za Habari Namba 12 ya mwaka 2016, Sera ya Habari na Utangazaji ya mwaka 2003 na Sera ya Taifa ya TEHAMA ya mwaka 2016 ambazo pamoja na mambo mengine zinaelekeza kuweka mazingira wezeshi ya kukuza maudhui ya ndani (Local content).